

Picha hii inamuonesha Suarez akikenua meno bila kufanikiwa kutekeleza kitendo chake cha kumng'ata Chiellini, tofauti na Chiellini mwenyewe alivyolalamika kuwa Suarez alimng'ata. Licha ya kuwa Suarez hakumng'ata Chiellini lakini anaweza kupewa adhabu na FIFA kwa dhamira aliyokuwa nayo ya kutaka kung'ata. Taarifa ya FIFA inasema bado wanaendelea kufanya uchunguzi na pindi watakapomaliza watatoa taarifa. Kama Suarez atapewa adhabu kutokana na kitendo hiki ataiathiri vibaya timu yake ya taifa kwani yeye ndiye mchezaji tegemezi kwenye safu ya ushambualiji.


No comments:
Post a Comment