Thursday, April 4, 2013

Yaya Toure amesaini mkataba mpya leo


Kiungo wa Man City Yaya Toure leo amesaini mkataba mpya na club yake baada ya vuta nikuvute ya wiki mbili. Yaya Toure aliomba mkataba mpya mwishoni mwa mwezi uliopita lakini club yake ilikuwa na kigugumizi hadi kupelekea kutoelewana kati ya Seluk wakala wa Toure na uongozi wa Man City. Hatua hiyo ili sababisha wakala huyo kukasirika na kutamka hadharani kuwa Toure yupo tayari kuhama City kama mkataba mpya utashindikana. Kufuatia hali hiyo, Club nyingi zikiwemo Chelsea na Madrid walionesha nia ya kumnunua Yaya lakini leo imekuwa mwisho wa yote baada ya Toure kukubaliana na City kwa kusaini mkataba wa miaka minne wenye thamani ya paundi milioni 11.

No comments:

Post a Comment