Shirikisho la mpira duniani FIFA limetoa onyo kwa Brazil
kuhusu ukamilikaji wa viwanja vitakavyotumika kwenye fainali za kombe la dunia
mwaka 2014. FIFA imesema haitabadilisha msimamo wake wa kuitaka Brazil iwe imekamilisha
viwanja vyote desemba mwaka huu 2013. Kauli hiyo ya FIFA imekuja kwasababu hadi
sasa viwanja sita bado havijakamilika na mategemeo ya kukamilika ndani ya mwaka
huu ni madogo. Viwanja ambavyo bado havijakamilika ni pamoja na Cuiaba, Manaus, Natal, Curitiba, Porto Alegre
na Sao Paulo. Vilevile FIFA imesema viwanja vyote vinatakiwa kujaribishwa
mara mbili vikiwa vimejaa watu kabla havijatumika kwenye kombe la dunia. Uwanja
ambao ulikuwa kwenye matengenezo na kukamilika ni Maracana tu ambao
ulizinduliwa mwezi wanne na ndiyo utakao tumika kwenye mechi ya fainali. Fainali
za kombe la dunia zitaanza tarehe 2 mwezi Juni 2013 na zitafanyika kwenye miji
12 kama inavyoonekana kwenye ramani.
No comments:
Post a Comment