
Mchezo ulianza kwa kasi tokea mwanzo hadi mwisho ukiwa ni wa mashambulizi ya pande zote lakini Man utd walionesha kuzidiwa hadi kupelekea Man city kujipatia magoli mawili. Udhaifu wa safu ya ulinzi ya Man utd umejionesha wazi ambapo Jones alishindwa kabisa kuliziba pengo la Vidic, vilevile washambuliaji wa Man utd akiwemo Rooney na Van Persie hawakuweza kuonesha mchezo mzuri ambao ulitarajiwa na mshabiki wa Man utd kwani walishindwa kabisa kupita kwenye ngome ya Man city. Matokeo ya mechezo huu umeifanya Man utd iendelee kungojea hadi mechi za mwisho ili kujihahakikisha ubingwa baada ya Man city kupunguza gepu kutoka tofauti ya pointi 15 hadi pointi 12.
No comments:
Post a Comment