Wakati Hispania ikiendelea kutafakari kwanini Barca na Real
zilifanya vibaya sana dhidi ya wapinzani wa Bundesliga, Bayern na Dortmund,
nchini Ujerumani Wajerumani wanaota "Der Klassiker“ yani fainali kati ya
Bayern na Dortmund itakayochezwa katika uwanja wa Wembley jijini London mnamo
Mei 25. Rais wa shirikisho la soka Ujerumani (DFB) Wolfgang Niersbach
amesema Bayern na Dortmund zimedhihirisha kiwango cha juu cha soka la Ujerumani
na kwamba Wajerumani kwasasa wanajipanga kwenye Wembley kushangilia fainali ya
timu mbili zikiwa zote ni za Ujerumani. Naye kocha wa timu ya taifa ya
Ujerumani "Die Manshaft“ Joachim Löw amesema wachezaji wake 14 waliopo
kwenye nusu fainali ya UEFA pamoja na Mesut Ozil na Sami Khedira wa Real
Madrid, unakifanya kikosi cha Ujerumani kuimarika zaidi husani katika kipindi
hiki cha kuelekea kombe la dunia litakalofanykia nchini Brazil mwakani. Bayern
Munich na Dortmund zikiwa zote ni timu za Ujerumani katikati ya wiki hii
ziliweza kuibuka na ushindi mnono wa magoli manne dhidi ya wapinzani wao Barcelona
na Real Madrid za Uhispania jambo ambalo linajumuishwa kwa kusema Ujerumani 8-1
Uhispania. Mchezo wa marudiano unatarajiwa kufanyika wiki ijayo ikiwa wapenzi
wa soka wanangojea kuziona timu za Ujerumani kusonga mbele.
No comments:
Post a Comment