Thursday, April 4, 2013

Ndolanga - Nitawaeleza ukweli wajumbe wa FIFA


Wajumbe wa FIFA wanatarajiwa kufika nchini April 16 mwaka huu kutathimini na kutolea maamuzi mgogoro ulioibuka ndani ya TFF kuhusu uchaguzi mkuu. Ndolanga ambaye ni mjumbe wa kudumu wa shirikisho hilo amesema ataeleza ukweli wote kuhusu matatizo yaliyopo TFF. Ndolanga alisema, wao kama TFF watahojiwa na sisi kama wadau tutahojiwa, ikifika zamu yangu nitaeleza ukweli wote bila kuficha, "haiwezekani TFF wafanye madudu na sisi tukae kimya". Ndolanga aliyasema hayo alipokuwa akiongea na waandishi wa habari, lakini hakutaka kusema ni mambo gani atawaeleza FIFA. 

No comments:

Post a Comment