Wednesday, April 3, 2013

Simba kufanya mkutano mkuu mwezi July


Uongozi wa Simba umesema utafanya mkutano mkuu July mwaka huu. Maamuzi hayo yamefikiwa katika kikao kilichoongozwa na mwenyekiti wake Aden Rage. Katika taarifa zake, uongozi wa Simba umesema tarehe halisi ya kufanya mkutano huo itatangazwa muda ukikaribia. Uongozi wa Simba umefikia hatua hii baada ya baadhi ya wanachama wake kufanya mkutano mwezi uliopita, mkutano ambao ulisemekana kuwa ni batili na kuchagua viongozi wapya. Katika mkutano mwezi July, wanachama wa Simba watakutana ili kuzungumzia maswala muhimu ya club hiyo ikiwemo matokeo mabovu ya club hiyo kwenye ligi kuu Tanzania bara.  

No comments:

Post a Comment