TPSC |
Baada ya kukaa kwa muda mrefu bila ya ushindi dhidi ya Chuo
cha Mtakatifu Agustino tawi la Mtwara (SAUT), Chuo cha Utumishi wa umma (TPSC)
kimeweza kutoka na ushindi wa goli 2-1 dhidi ya SAUT katika mchezo wa mpira wa
miguu uliofanyika kwenye uwanja wa Nangwanda mkoani Mtwara katika fainali ya
Pro Life Competition 2013. Timu hizi mbili ndiyo zenye upinzani wa juu kwenye michuano hii na kawaida SAUT ndiyo watetezi wa kombe hili, lakini mwaka huu TPSC walijipanga vizuri na kuweza kuwadhibiti ipasavyo SAUT tokea mwanzo wa mchezo hadi mwisho. Michuano hii ambayo ni maarufu mkoani Mtwara
inadhaminiwa na Father Aidan Msafiri ambaye ni mkufunzi katika chuo cha SAUT
tawi la Mtwara. Chuo cha TPCS kiliingia fainali baada ya kukifunga chuo cha
Uhasibu (TIA) tawi la Mtwara wakati SAUT waliingia fainali baada ya kuwatoa
Naliendele Mtwara ambao ni kikosi cha jeshi kutoka jeshi la wananchi wa
Tanzania tawi la Mtwara. Wakati huo huo,
kwa upande wa mpira wa pete SAUT tena ilipokea kichapo kutoka kwa TPSC lakini kwa
upande wa volleyball SAUT iliweza kutetea kombe dhidi ya TPSC. Baada ya michezo
hii kuisha baadhi ya wanafunzi wa chuo cha SAUT wamekiri kuondoka kwa
wanachuo wenzao waliokuwa mwaka wa tatu kumezifanya timu zao kuwa dhoofu
kwasababu hawakuwa wamejiandaa kupokea kijiti kutoka kwa wenzao waliomaliza.
Michuano hii ya Pro Life inayodhaminiwa na Father Msafiri ilianzishwa ikiwa na
dhumuni la kuwakutanisha pamoja wanavyuo na watumishi wa umma mkoani Mtwara ili
kujenga umoja baina yao lakini vilevile kuendeleza michezo ndani ya mkoa na
kuwafanya vijana wapate shughuli zingine za kufanya baada ya masomo na kazi ili
kujiepusha na vishawishi vinavyopelekea maambukizi ya ukimwi.
No comments:
Post a Comment