Wednesday, July 10, 2013

Quinton Fortune wa Man utd atembelea Azam Fc leo

Mchezaji wa zamani wa Man utd Quinton Fortune leo ametembelea Azam Complex kujionea uwekazaji wa klabu hiyo katika soka. Fortune kwa sasa anasomea ukocha wa soka kwenye shule ya Manchester United, ziara yake ya leo ilikuwa maalumu kutembelea Azam FC Chamazi kwa mwaliko wa DHL. Fortune ameipongeza Azam FC kwa uwekezaji walioweza kuufanya hadi sasa na kusema ni maendeleo makubwa katika soka ambayo yataisaidia Tanzana katika siku zijazo. 

No comments:

Post a Comment