Mshika kibendera Musa Kadyrov wa nchini Urusi amefungiwa maisha
kuchezesha mechi nchini humo baada ya kumshambulia kwa ngumi na mateke mchezaji
wa Amkar Perm, Ilya Krichmar. Musa alifanya kitendo hicho mara tu mwamuzi wa kati kupuliza filimbi ya mwisho kumaliza mchezo. Kijana huyo aliyeshambuliwa alisema ‘ mshika kibendera huyu
amekuwa akichezesha vibaya mechi nyingi zikiwemo za kwetu, ila mimi sijawahi
kumsema vibaya popote, sasa sijui kwanini alinipiga mimi, nawashukuru wachezaji
wenzangu waliokuja kunisaidia, angeniumiza kwa hasira aliyokuwa nayo’. Matukio
kama haya ya waamuzi kuwapiga wachezaji ni nadra sana kutokea kwani wao
wanasimama kama wasuluhishi wa mchezo hivyo ni kosa kubwa kushiriki katika
kuvunja sheria za soka.
Video ya tukio hilo
No comments:
Post a Comment