Monday, April 29, 2013

Mwamuzi afungiwa kuchezesha maisha Russia

Mshika kibendera Musa Kadyrov wa nchini Urusi amefungiwa maisha kuchezesha mechi nchini humo baada ya kumshambulia kwa ngumi na mateke mchezaji wa Amkar Perm, Ilya Krichmar. Musa alifanya kitendo hicho mara tu mwamuzi wa kati kupuliza filimbi ya mwisho kumaliza mchezo. Kijana huyo aliyeshambuliwa alisema ‘ mshika kibendera huyu amekuwa akichezesha vibaya mechi nyingi zikiwemo za kwetu, ila mimi sijawahi kumsema vibaya popote, sasa sijui kwanini alinipiga mimi, nawashukuru wachezaji wenzangu waliokuja kunisaidia, angeniumiza kwa hasira aliyokuwa nayo’. Matukio kama haya ya waamuzi kuwapiga wachezaji ni nadra sana kutokea kwani wao wanasimama kama wasuluhishi wa mchezo hivyo ni kosa kubwa kushiriki katika kuvunja sheria za soka.  
Video ya tukio hilo 

No comments:

Post a Comment