Sunday, March 31, 2013

Kocha wa Simba amwaga machozi


Kocha mkuu wa timu ya Simba, Patrick Liewig alimwaga machozi kwenye hotel waliyofikia jijini Mwanza baada ya mchezo kati ya Toto na Simba kuisha. Katika mchezo huo timu hizo zilitoka sare ya goli mbili kwa mbili. Kocha huyo alisema inamuuma sana kuona Simba inatoka droo kwenye mchezo ambao walikuwa na uwezo wa kushinda. Kocha Liewig alisema ulikuwa ni uzembe tu wa mabeki, wachezaji hawachezi kwa moyo mmoja, itabidi tukae pamoja wachezaji na uongozi ili tuweze kujadili hali hii ya Simba, matatizo mengi ya timu yanaanzia kwenye uongozi sio wachezaji pekee (hisani ya gazeti la mwananchi)

No comments:

Post a Comment