Thursday, April 4, 2013

Ferguson amtetea Robin Van Persie


Kocha wa Man Utd Sir Alex ametetea mshambualiji wake tegemezi Robin Van Persie kuwa hajaishiwa kiwango. Sir Alex akiongea kupitia United Magazine alisema “Robin bado hatujaweza kumtumia vizuri lakini sio kwamba amekwisha kiwango, ni mazingira yetu sisi kama United ndiyo yamemfanya kasi yake ipungue ila atarudi muda sio mrefu”. Sir Alex alieleza hayo kwa kile kinachosemwa kuwa Robin Van Persie anasumbuliwa na msongo wa mawazo kwavile hajafunga goli tokea February 10 baada ya mechi na Evarton. Van Persie huu ndiyo msimu wake wa kwanza na Man utd akitokea Arsenal kwa dau la paundi milioni 24, hadi sasa ameshacheza mechi 31 na kufunga magoli 23. 

No comments:

Post a Comment