Wednesday, April 17, 2013

Leonel Messi yupo fiti kucheza dhidi ya Bayern Munich

Mshambuliaji tegemezi wa Barcelona Lionel Messi anategemewa kucheza kwenye mechi ya nusu fainali ya kwanza kati ya Bayern Munich na Barcelona inayotarajiwa kufanyika wiki ijayo jijini Munich. Messi aliyepata maumivu ya misuli kwenye mguu wake wa kulia katika mechi ya kwanza kati ya PSG na Barcelona amekuwa kwenye matibabu kwa kipindi cha wiki tatu sasa licha kucheza kipindi cha pili katika mechi ya marudiano dhidi ya PSG. Messi alipewa taarifa za kupona kwake kutoka kwa daktari wa klabu akiwa kwenye mazoezi jumanne ya wiki hii. Messi ameshakosa mechi mbili za ligi na anatarajiwa kutokucheza mechi yoyote akingojea mechi dhidi ya Bayern Munich ili kuepusha majeraha ya aina yoyote kwa mchezaji huyo ambaye ni chachu kwa Barcelona kupata ushindi.  

No comments:

Post a Comment