Wednesday, April 17, 2013

Real Madrid yaipita Man utd kwa utajiri

Klabu ya Man utd imepoteza nafasi yake ya kwanza kama klabu ya mpira wa miguu tajiri kuliko zote duniani na nafasi yake kuchukuliwa na Real Madrid. Taarifa za Forbes wiki hii zinasema Man utd imekuwa namba moja toka mwaka 2004 lakini mwaka huu imeshuka kwa mara ya kwanza tokea Forbes waanze kuthaminisha vilabu vya soka duniani. Real Madrid imeweza kuipiku United kwa kufikisha mapato ya paundi bilioni 2.15 kwa mwaka, wakati Man utd wakiwa nafasi ya pili ambapo mapato yao ni paundi bilioni 2.07. Barcelona wanashika nafasi ya tatu wakifutiwa na Arsenal nafasi ya nne wakati Bayern Munich wanashika nafasi ya tano. 
Santiago Bernabeu uwanja wa Real Madrid wenye uwezo kuchukua watazamaji 85,000 ni kiwanja cha tatu kwa ukubwa barani ulaya. Uwezo mkubwa wa kubeba watamaji wengi wa kiwanja hiki imesemakana kuwa ni sababu mojawapo ya Real Madrid kuwa klabu tajiri duniani kwa kupokea mapato mengi ya mlangoni ikilinganishwa na Man utd yenye uwanja unaoweza kubeba watazamaji 75,000. 
Real Madrid imeweza kuimarisha zaidi mapato yake kupitia mapato makubwa ya uwanjani, hakimiliki za kuonesha mechi zake na matangazo mbalimbali ya ndani na nje ya uwanja. Forbes imesema mbali ya Real Madrid kuizidi Man utd kwa tofauti ya fedha chache lakini Real Madrid imeonekana bado ni imara zaidi kiuchumi ikilinganishwa na United kwa kigezo kuwa imeweza kushika namba moja ikiwa bado inaweza kuwalipa mishahara mikubwa wachezaji wake kama Cristiano, Kaka na kocha wake Mourinho ambaye ndiye kocha anayelipwa zaidi ya makocha wote wa soka duniani ambapo malipo yake kwa mwaka ni paundi milioni 12.3 tofauti na Sir Alex Ferguson anayelipwa paundi milioni 7.6. Vilevile Real Madrid ndiyo klabu yenye historia ya kununua wachezaji kwa pesa nyingi kulizo zote duniani, ikikumbukwa uhamisho wa Cristiano Ronaldo wa dola milioni 80 ambao hadi leo ni rekodi ya dunia. 

Siku Cristiano Ronaldo alipotambulishwa rasmi kwa mashabiki wa Real Madrid baada ya kununuliwa kwa rekodi dola milioni 80 kutoka Man utd. Jumla ya mashabiki 80,000 waliijaa kwenye kiwanja kumkaribisha Ronaldo. 

No comments:

Post a Comment