Wednesday, April 17, 2013

Luis Suarez hatouzwa popote - Ayre

Mkurugenzi mtendaji wa klabu ya Liverpool Ian Ayre amesisitiza kuwa Luis Suarez hatouzwa mwishoni mwa msimu huu. Ayre aliyasema hayo alipohojiwa kuhusu tetesi zilizopo kuwa Suarez atauzwa kwenda Bayern Munich, PSG au Man City, Ayre alisema “ili Liverpool iweze kushinda kombe la ligi na kushiriki michuano ya ulaya lazima iwe na wachezaji kama Suarez na Gerrard, hivyo Liverpool haiwezi kumuuza Suarez, kwasasa tupo kwenye kipindi cha kuimarisha timu yetu, tumefanya usajili mzuri mwezi January, timu yetu imeimarika zaidi na tutaendelea kufanya usajili lakini sio kuuza wachezaji mahili kama Suarez. Suarez amehusishwa sana kuihama Liverpool katikati ya msimu huu baada ya Liverpool kufanya vibaya kwenye ligi kuu kitu ambacho kimeelezwa kuwa Suarez hajakifurahia hivyo atapenda kujiunga na klabu kubwa ili akuze zaidi kipaji chake na kushinda vikombe.   

No comments:

Post a Comment