Tuesday, April 2, 2013

Sababu mbili zilinifanya niende Arsenal na kuikacha United - Ramsey


Kiungo wa Arsenal, Ramsey amesema sababu kubwa iliyomfanya ajiunge na Arsenal na kuikacha Man Utd ni juhudi alizoonesha kocha wa Arsenal Arsene Wenger na mahusiano mazuri na wachezaji yalipo kwenye club hiyo. Ramsey alisema “ kocha Wenger alituma ndege binafsi kutoka London hadi Wales nilipokuwepo ili inichukue niende kuongea naye, nilipofika walinipokea vizuri na kunipeleka kwa Wenger ambapo alinipa mipango mizuri ya kukuza kipaji changu”. Mambo haya mawili ndiyo yalinifanya nije Arsenal na kuiacha United, kwani sikuwahi kufikiria kama club kubwa kama Arsenal inaweza kunitumia ndege binafsi na vilevile nilivutiwa sana na mipango mizuri niliyopewa na Wenger. Ramsey (22) alijiunga na Arsenal mwaka 2008 ameshacheza mechi 96 na magoli 7.

No comments:

Post a Comment