Thursday, May 16, 2013

Bye Bye Beckham, kustaafu mwaka huu

Winga wa PSG David Beckham ametangaza rasmi kustaafu soka mwishoni mwa msimu huu. Beckham mwenye umri wa miaka 38 ametangaza uamuzi huo leo akiwa ameshacheza zaidi ya mechi 100 na timu ya taifa, vikombe sita vya ligi kuu ya Uingereza akiwa na Man utd na vikombe vingine vitatu vya ligi ya Hispania, Marekani na Ufaransa akiwa na timu za Madrid, Galaxy na PSG. Beckham alianza kucheza soka akiwa na miaka 14 alipojiunga na Man utd mwaka 1993 hadi mwaka 2003 alipohamia Real Madrid na mwaka 2007 alihamia Galaxy nchini Marekani. Mwaka 2009 hadi 2010 alikwenda Ac Milan kucheza kwa mkopo  na mwaka 2013 alihamia PSG ambapo ameshacheza mechi tisa hadi sasa. Beckham hadi sasa ni mchezaji pekee barani Ulaya ambaye ameweza kushinda kombe la ligi na timu nne tofauti na pia ni mchezaji ambaye ameshacheza kwenye ligi tatu kubwa barani ulaya (ligi ya Uingereza, Hispania na Ufaransa).  Katika maneno yake na waandishi wa habari Beckham amesema “nashukuru nimeweza kucheza hadi muda huu, imefikia kipindi sasa niwaachie wengine kwasababu siwezi tena kucheza kwenye kiwango changu cha juu, nawashukuru PSG kwa kunisajili kwenye kipindi hiki lakini imefikia muda nipumzike kwenye soka ili niweze kufanya shughuli zingine”. Mbali na soka Beckham pia anafanya shughuli nyingi ikiwemo mitindo na kufanya matangazo mbalimbali ya bidhaa na huduma za makampuni. David Beckham na mkewe Victoria hadi sasa wana watoto wanne Brooklyn Joseph (alizaliwa 1999 London), Romeo James (alizaliwa 2002 London),  Cruz David (alizaliwa 2005 Madrid); na binti yao mmoja Harper Seven (alizaliwa 2011,Los Angeles) 

No comments:

Post a Comment