Klabu ya Simba imeendelea kupondwa na washabiki mbalimbali
wa soka nchini wakiwemo wa Yanga na wa timu zingine za ligi kufuatia mchezo wa
jumamosi wakisema Simba haina uwezo wa kuifunga Yanga. Hii imekuja kufuatia
uamuzi walioufanya klabu ya Simba kuamua kuwapa vijana nafasi ya kuonesha uwezo
wao kwani kikosi cha Simba kinachotarajiwa kushuka dimbani siku ya jumamosi
kitajaa wachezaji wadogo ambao wamesekana hawana uzoefu zaidi ya
wachezaji wa Yanga. Maneno hayo yalianzia kwa wazee wa Yanga ambao walitoa
kauli yao mbele ya waandishi wa habari wakisema “Mnyama ajiande kuuwawa
jumamosi” lakini vilevile kocha mkuu wa Azam kupitia Mwananchi alisema "Simba
inategemea nguvu ya mashabiki kushinda lakini sio uwezo wa wachezaji" na kauli
zinazolingana na hizi zimetolea vilevile na baadhi ya mashabiki wa Yanga. Kufuatia kauli
hizi viongozi mbalimbali wa Simba akiwemo mwenyekiti Aden Rage amewahakikishia
wapenzi wa Simba wasiwe na wasiwasi kwani vijana wapo tayari kuiangamiza Yanga
na kusisitiza wajitokeze kwa wingi siku ya jumamosi. Mbali na kauli hii ya rage na viongozi wengine wa Simba lakini bado wadau wengi wa soka
nchini hawajiridhishi ndani ya fikra zao kuwa Simba itaweza kushinda
mchezo dhidi ya Yanga kwa kutumia vijana wadogo licha yakuwa wanaamini inaweza
kutokea muujiza Yanga wakafungwa, hivyo mchezo huo wa jumamosi kati ya Simba na Yanga unangojewa na wengi ili kutegua maswali yanayowazunguka wadau wa soka nchini.
No comments:
Post a Comment