Shirikisho la mpira wa miguu duniani FIFA bado lipo kwenye
kigugumizi kuhusiana na miezi itakayotumika kufanya kombe la dunia la mwaka
2022 nchini Qatar. Kigugumizi cha FIFA kinakuja kutokana na hali ya joto la
nchi ya Qatar kipindi cha mwezi wa watano hadi wa saba miezi ambayo kombe la
dunia huwa linafanyika. Nchi ya Qatar huwa ina joto linalofikia digrii 50
kuanzia mwezi wa tano hadi wa saba kitu ambacho kitaadhiri michuano hiyo. Mwezi
uliopita nchi ya Qatar ilithibitsha kuwa hakutakuwa na tatizo lolote kuhusiana
na jambo hilo kwani wameshapata teknolojia ya kupooza joto kwenye viwanja lakini
wadau wengi wa soka wamepinga kauli hiyo ya Qatar wakisema teknolojia hiyo
itaweza kupoza joto ndani tu ya viwanja lakini nje kutakuwa na joto. Wadau wamehoji
swala hili kwasababu kombe la dunia linaambatana na vitu vingi ikiwemo michezo
mbalimbali nje ya viwanja na mitaani kitu ambacho kitawaadhiri sana mashabiki. Vilevile, timu nyingi zinapendelea kufanya mazoezi kwenye viwanja vya wazi ambavyo
haiwezekani kuweka viyoyozi hali ambayo itazifanya timu zote kufanya mazoezi
kwenye viwanja vya ndani. Kutokana na hali hii baadhi ya wadau wa soka wakiwemo
baadhi ya viongozi wa FIFA wamependekeza michuano hiyo ifanyike mwezi novemba
na disemba kitu ambacho kitaadhiri michuano ya ligi mbalimbali duniani ambayo
hufanyika kuanzia mwezi wa nane hadi wa tano. Hali hii ndiyo inaifanya FIFA
hadi leo ibakie na kigugumizi cha kuamua kama kombe la dunia litafanyika kwenye
miezi ya kawaida au itabadilishwa. Sepp Blatter raisi wa FIFA yeye ameendelea
kusimama na msimamo wake kuwa michuano hiyo itafanyika miezi ile ile (wa tano hadi wa saba) lakini msimamo wake unakuja ili kulinda maamuzi ya kamati kuu ya FIFA
iliyotoa uamuzi michuano hiyo ifanyika Qatar, uamuzi ambao umeonekana kuwa na
dosari. Midahalo na vikao vingi vimeshafanyika kujadili swala hili lakini hadi leo jibu halijapatika, lakini jibu lazima lipatikane kwasababu michuano hiyo lazima itafanyika.
No comments:
Post a Comment