Thursday, May 9, 2013

Madrid watoswa kumchukua Neymar kwa €100m

Raisi wa Real Madrid Florentino Perez alikuwa tayari ameandaa kiasi cha Euro milioni 100 ili kumsajili mshambuliaji wa Santos Neymar lakini wakala wa Real Madrid katika masuala ya usajili aligonga kisiki baada ya Neymar kumkatalia. Neymar ambaye anatabiriwa kuwa moja kati ya mastaa wakubwa kwenye soka dunia baada ya kombe la dunia mwaka 2014, amekuwa akihitajika na klabu nyingi za ulaya ikiwemo Real Madrid, Barcelona, PSG, Bayern na Chelsea. Lakini kati ya vilabu hivi Barcelona na Real Madrid ndivyo vinapewa nafasi kubwa zaidi ya kumsajili kutokana na uwezo wa kifedha walikuwa nao. Barcelona walitoa ofa ya Euro mil 45 mwaka juzi 2011 ili kumsajili Neyamar, na kiasi hicho kilikubaliwa kwa mashariti kwamba mchezaji huyo atahamia Barca baada ya kombe la dunia mwaka 2014, lakini, Real Madrid wiki hii waliamua kuongeza pesa mara mbili zaidi ya Barcelona ili kumnasa Neymar kwasababu wanaogopa mchanganyiko wa Messi na Neymar utawaletea upinzani mkali zaidi. Vilevile kuna tesitesi kuwa Cristiano Ronaldo anaweza kuondoka Madrid mwishoni mwa msimu huu hivyo Real Madrid wanatafuta mbadala wake ambaye wanafikiria Neymar ataweza kuziba pengo la Cristiano. Lakini Real Madrid bado wana wakati mgumu kuweza kumsajili Neymar kwasababu mchezaji huyo ameshasaini mkataba wa mwanzo na Barcelona na vilevile Neymar mwenyewe ameshaonesha nia ya kujiunga na Barcelona ili kucheza pamoja na Messi, Iniesta na Xavi.  

No comments:

Post a Comment