Thursday, March 28, 2013

Mancini achukizwa na Wilmots kwa kumchezesha Kompany


Kocha wa Man City Roberto Mancini amechukizwa na kitendo cha kocha wa Belgium Marc Wilmots kumchezesha beki wa Man City Vicent Kompany. Mancini akiongea na BBC sport amesema, Kompany ameondoka hapa bado hajapona na hajacheza mechi yoyote toka January, lakini yeye Wilmots amemchezesha dakika zote 90 bila kuomba ushauri kwa madaktari wa Man City, nafikiri baadhi ya makocha wa timu za taifa lazima waelewe kuwa hawa wachezaji ni wanadamu pia. Kompany ameondoka hapa akiwa bado hajapona inawezekanaje ndani ya wiki moja awe amepona? alihoji Mancini. Kompany aliumia mwezi wa kwanza kwenye ya FA kati ya Man city na Stoke. 


No comments:

Post a Comment