Saturday, April 13, 2013

Juan Mata amekiri Yaya Toure ni kiungo bora

Kuelekea kwenye mchezo wa nusu fainali ya FA cup, Juan Mata kiungo wa Chelsea amemfagilia Yaya Toure wa Man city kuwa ni kiungo aliyekamilika. Mata alisema “ Yaya ni kati ya viungo bora duniani, anaweza kuzuia, kushambulia na kufunga, ni mchezaji mwenye nguvu na pia mrefu, kwa kweli ana kipaji cha kipekee sana, tutahitaji nguvu za ziada kumzuia. Chelsea tuna viungo na mabeki wazuri tutaweza kumzuia licha yakuwa atatusumbua”. Mata aliyasema hayo alipokuwa akihojiwa na jarida la “The Sun” kufuatia mchezo wa jumapili ambao ni muhimu sana kwa timu zote Chelsea na Man city ikiwa kila timu inahitaji ushindi ili iweze kuweka heshima baada ya kukosa kombe la ligi na UEFA champions.  

No comments:

Post a Comment