Saturday, April 13, 2013

Hernandez - Nitaendelea kuwa mnyenyekevu

Mshambuliaji wa Man utd Javier Hernandez baada ya kukaa kimya kwa muda mrefu amejitokeza wikiendi hii na kusema yeye atapigana hadi arudishwe kwenye kikosi cha kwanza hata kama Falcao na Lewandowski watasajiliwa na United. Hernandez ameyasema hayo alipokuwa akiongea na Dailymail baada ya fununu kuwepo kwamba Man utd italipa keshi paundi milioni 48 pamoja na Hernandez juu kwa klabu ya Atletico Madrid ili kumnunua Falcao. Alipouliza kuhusu hilo Hernandez alisema "hiyo ni mipango ya klabu, ila mimi nitapigana nibakie Man utd hata kama United italeta mshambuliji mwingine, wachezaji wengi wanapenda kuwepo United, mimi nimepata nafasi hii lazima niitumie vizuri, hivyo nitaendelea kuwa mnyenyekevu na kuheshimu maamuzi ya kocha wangu kila siku”. Hernandez (24) yupo kwenye wakati mgumu kurudi  kwenye kikosi cha kwanza kutokana na ushindani mkali kutoka kwa Van Persie, Rooney na Welbeck. Hadi sasa Hernandez ameshacheza mechi 15 kati ya mechi 31 za ligi na amefunga magoli nane hadi sasa.   

No comments:

Post a Comment