Klabu ya Chelsea imewasili jijini Bangkok nchini Thailand leo tayari kuanza ziara yake kwenye nchi za Asia. Jose Mourinho ndiye amekuwa kivutio kikubwa kuliko wote kwenye mapokezi ya timu kutokana na mapenzi yake kwa mashabiki wa Chelsea. Mashabiki wengi wa Chelsea wameonesha imani kwa Jose ambaye amejiunga tena na The blues mwaka huu. Kuwasili kwa Chelsea nchini Thailand kumeleta msisimko zaidi kwa wapenzi wa soka wa nchi hiyo, kwani Man utd pia ipo nchini Thailand kwa ziara ya wiki moja, hivyo mashabiki wa kila upande wanashindana kwa namna tofauti ikiwemo kuvaa jezi kwa wingi na kushangilia mitaani. Hadi sasa hali inaonesha ngoma ni droo kati ya mashabiki wa Man utd na Chelsea kwa kulinganisha idadi ya watu waliojitokeza kwenye mapokezi ya timu hizi mbili. Zifuatazo ni picha za mapokezi ya Chelsea leo hii
No comments:
Post a Comment