Picha hii inaonesha habari kutoka kwenye mtandao wa Marca unaoripoti kuwa Juan Mata atavaa jezi namba 7 akiwa na timu yake mpya ya Man utd. Jezi hii imeshawahi kuvaliwa na wachezaji wengi maarufu ndani ya klabu hiyo akiwemo Beckham, Cristiano Ronaldo, Contona na Best. Wachezaji hawa wanne waliweza kuitendea haki namba hii na kuifanya iwe jezi kwa wachezaji maalum. Swali linakuja ,Je Mata ataweza kuipa heshima namba hii au itakuwa kubwa kama ilivyokuwa kwa Michael Owen akashindwa kuitendea haki???? Yetu Machooo
No comments:
Post a Comment