Wachezaji wa Galatasaray wakiongozwa na Didier Drogba wakiwasili nchini England tayari kukipiga na Chelsea siku ya jumanne kwenye michuano ya Uefa champions. Timu ya Galatasaray iliwasili mida ya kumi jioni jumapili kwenye uwanja wa ndege wa Heathrow na kupokelewa na kundi kubwa la mashabiki waliokuwa wamekusanyika kwenye uwanja. Mechi baina ya timu hizi mbili inategemewa kuwa na mvuto wa aina yake ikiwemo kurudi kwa Drogba ndani ya Stamford Bridge akiwa na timu pinzani. Uzuri wa mechi hii pia unakuja kutokana na matokeo ya awali ambapo timu hizi mbili zilitoka droo ya goli 1-1 jambo ambalo litazifanya timu zote kucheza mpira wa kushambulia. Timu ya Chelsea inapewa nafasi kubwa ya kushinda mchezo huu licha ya kuwa Galatasaray sio timu ya kubeza.
Mashabiki wa Galatasaray waliokusanyika kwenye uwanja wa ndege kuwapokea wachezaji
No comments:
Post a Comment