Tuesday, April 30, 2013

Video highlights Real Madrid 2-0 Dortmund


Maneno ya Jose Mourinho baada ya Madrid kutolewa

Baada ya mechi kuisha huku Real Madrid wakitolewa kwenye michuano ya UEFA Jose Mourinho alihojiwa kuhusiana na mechi na kusema, 'tumecheza vizuri sana, wachezaji wamecheza kwa nguvu moja mwanzo hadi mwisho lakini siwezi kusahau mechi ya kwanza, tuliyocheza Ujerumani, tulicheza vibaya sana, Dortmund walinipa adhabu kubwa mno na tumetoka kwasababu ya adhabu ya goli 4-1. Vilevile nimesikitishwa sana na refa wa leo hajatoa kadi kwenye faulo nyingi hususani penati tulizopata bila yeye tungekuwa fainali muda huu. Alipoulizwa kuhusu uwepo wake Real Madrid msimu ujao Mourinho alisema, napenda kuwepo mahali ambapo watu wananipenda na wanafurahia uwepo wangu kwahivyo nitakuwepo mahali ninapopendwa, ikiwa ni ishara ya wazi kabisa kuwa msimu huu ndiyo mwisho wake Real Madrid kwani watu wa Real wamekuwa wakimponda sana Mourinho wakisema amewaharibia mpira wao.  

Real Madrid wametolewa kiume kwa magoli 3-4 BVB

Timu ya Real Madrid imetolewa kwenye michuano ya UEFA champions na Dortmund baada ya ushindi wa magoli finyu 2-0 hivyo kuiwezesha Dortmund kusonga mbele na kuingia fainali kwa jumla wa magoli 4-3. Real Madrid ilicheza mchezo mzuri wa kuvutia na kwa kasi kubwa tokea mwanzo hadi mwisho wa mchezo lakini safu yake ya ushambuliaji haikuwa makini kumalizia mipira ya mwisho. Cristiano Ronaldo, Higuain, Ozil, Kaka na Di Maria wamechezea nafasi nyingi sana ambazo kama wangezitumia vizuri basi Real Madrid wangeweza kutoka kifua mbele kwa magoli mengi. Golikipa wa Dortmund pia alionesha umahiri wake mkubwa sana baada ya kuokoa mipira mingi ambayo ilikuwa ni magoli ya wazi. Katika mahojiano kabla ya mechi Jose Mourinho kocha wa Real Madrid alisema watakwenda kupigana kufa na kupona na kucheza kwenye kiwango chao cha juu kuliko siku zote, ni kweli wachezaji wa Real wametekeleza aliyosema Jose lakini umahiri wa mabeki wa Dortmund ndiyo umeifanya timu hiyo iweze kuhimili mikiki ya Real Madrid. Hivyo hadi mwisho wa mchezo Real Madrid 3-4 Dortmund. Mchezo mwingine wa nusu fainali utachezwa leo usiku jumatano kati ya Barcelona na Bayern Munich, ikiwa pia ni mchezo wa "mission impossible" kwa Barcelona kwani watahitajika kuwafunga Bayern magoli matano kwa bila ili wafuzu jambo ambalo matokeo yake yanawezekana kimahesabu kuliko kiuhalisia. Magoli yalifungwa na Benzema 83, Sergio Ramos 89. 

Vikosi vya timu zote mbili

Real Madrid: Diego Lopez, Essien, Ramos, Varane, Coentrao (Kaka 57); Xabi Alonso (Khedira 67), Modric; Di María, Özil, Cristiano Ronaldo, Higuaín (Benzema 57)

Borussia Dortmund: Weidenfeller; Piszczek, Subotic, Hummels, Schmelzer; Bender (Santana 90), Gundogan; Gotze (Grosskreutz 14), Reus, Blaszczykowski; Lewandowski (Kehl 87)

Is it on? Sergio Ramos makes it 2-0 and gives Madrid hope
Benzema na Ramos wakishangilia goli la kwanza la Real Madrid lililogungwa na Benzema dakika ya 83
Wrestle for the ball: Real Madrid players fight with Dortmund's goalkeeper Roman Weidenfeller after the first goal
Ronaldo, Benzema na Ozil wakigombania mpira dhidi ya goli kipa wa Dortmund baada ya goli la kwanza kufungwa, golikipa wa Dortmund aling'ang'ania mpira ili kupoteza muda
Down and out: Ronaldo gestures after being knocked to the floor
Ronaldo akinyoosha mikono kuomba penati baada ya kuangushwa katika dakika ya 92 ya mchezo, lakini refa hakutoa penati kwasababu aliangushwa hakiwa bila mpira
No way Jose: Mourinho shows his frustration on the sidelines
Mourinho akishangaa pia kufuatia kitendo cha refa kugomea penati baada ya Ronaldo kuangushwa chini dakika ya 92
End of the road: Ronaldo walks on the pitch looking dejected
Cristiano Ronaldo akitoka nje wa uwanja kwa masikitiko baada ya mchezo kumalizika kwa matokeo ya jumla Real Madrid 3-4 Dortmund
HANDBAGS ... Sergio Ramos has a friendly word with Robert Lewandowski
Vita ilikuwa kali kati ya Ramos na Lewandowski, katika mchezo uliopita Jose Mourinho alisema mabeki wake hawamkufanyia rafu za kutosha Lewandowski ndiyo maana aliwafunga magoli mengi, akasema mchezo wa marudiano vijana wake watamchezea rafu za kutosha Lewandowski kitu ambacho walikitekeleza, ikiwemo kumpiga viwiko, kumkanyaga na kumsukuma

Jason Collins ajitangaza rasmi kuwa ni shoga


Mchezaji wa Washington Wizards Jason Collins ametangaza rasmi kuwa yeye ni shoga baada ya uvumi wa muda mrefu. Jason alijitangaza kwenye jarida la Sports Illustrated lililomnukuu akisema ‘Mimi nina umri wa miaka 34, mchezaji mweusi wa NBA ni shoga’, taarifa hizi zimelipuka kwenye vyombo vya habari nchini Marekani kwani sio jambo la kawaida kwa mchezaji wa NBA kujitangaza hadharani kuhusu ushoga. Jason katika mahojiano na ABC News leo asubuhi amesema, baada ya kujitangaza hadharani anajisikia kuwa huru na mwenye furaha sana. Kufuatia kauli hiyo ya kujiweka hadharani, watu wengi maarufu nchini Marekani  akiwemo rais mstaafu Bill Clinton na mchezaji mwenzake Kobe Bryant wamempongeza Jason kwa uamuzi wake na wametoa ombi kwa wachezaji wengine kufuata nyayo za Jason. Lakini uchambuzi umeonesha kuwa licha ya Marekani kuwa mbele kimaendeleo ya jamii hususani uhuru wa kuongea na kudumisha haki za binadamu lakini bado itakuwa vigumu kwa wachezaji wote ambao ni mashoga kujitangaza kwasababu wanahofia kubaguliwa, kuzomewa na hata kukosa huduma zingine kama mashoga. Nchi nyingi barani Ulaya na Amerika zimekuwa zikihamasisha kukubalika kwa ushoga ikiwa ni sera za kisiasa ili kushinda chaguzi mbalimbali lakini ndani ya jamii zenyewe za wa Amerika na Ulaya bado jambo hili la ushoga halijakubalika katika jamii yote. Vilevile, jamii kubwa inachukulia mtu shoga kama ni dhaifu hivyo kwa wanamichezo ambao wanatakiwa kuwa wakakamavu itakuwa vigumu sana kujitangaza kuwa ni mashoga kwani ajira zao zinaweza kuzorota na pia kupoteza mashabiki. Jason Collins mwenye urefu wa futi 7 kabla ya kujiunga na Washington Wizards mwaka huu ameshacheza kwenye timu kubwa za NBA zikiwemo Boston Celtics, Atlanta Hawks, Memphis Grizzlies, Minnesota na New Jersey Nets. 

TFF yatoa hati ya uhamisho kwa Yusuf

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limetoa Hati ya Uhamisho wa Kimataifa (ITC) kwa mchezaji Yusuf Kunasa kucheza nchini Msumbiji. Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini Msumbiji (FMF) lilituma maombi TFF kumuombea hati hiyo Kunasa anayekwenda kujiunga na timu ya Estrela Vermelha da Beira inayocheza Ligi Kuu nchini humo. Kunasa ambaye msimu huu hakuwa na timu (free agent) amejiunga na timu hiyo akiwa mchezaji wa ridhaa (amateur). Zaidi ya wachezaji kumi kutoka Tanzania hivi sasa wanacheza katika klabu mbalimbali nchini Msumbiji. Timu ya Estrela Vemalha hadi sasa inashika nafasi ya kumi kwenye ligi ya msumbiji ikiwa imecheza mechi sita, imeshinda miwili, droo moja na imepoteza michezo mitatu sio timu kubwa nchini Msumbiji kwani ilishuka daraja mwaka 2008 na kwasasa ipo kwenye kipindi cha kujiimarisha kwani miaka ya 80 ilishawahi kuiwakilisha Msumbiji kwenye michuano ya Afrika pamoja na kushinda kikombe cha jijini la Mputo mwaka 2010.   

Mechi za ligi kuu Tanzania bara wiki hii 1/5/13

Yanga Sc vs Coastal Union

Mtibwa Sugar vs African Lyon

Polisi Moro vs Kagera Sugar

JKT Ruvu vs Tanzania Prisons

Ruvu Shooting vs JKT Oljoro

Brandts,tutaendeleza ushindi mechi zilizosalia

Kocha mkuu wa Yanga mholanzi Ernie Brandts amesema pamoja na kuwa tayari wameshatangazwa mabingwa wapya, bado kikosi chake kitashuka dimbani kuhakikisha kinaendeleza wimbi la ushindi wa kusaka pointi tatu katika michezo iliyosalia.Brandts alisema "Wengi wanaona kwa kuwa tumeshatwaa ubingwa basi tutapunguza kasi ya ushindi, hilo kwetu hakuna, tunaendelea na mazoezi kujiandaa kuhakikisha tunashinda michezo yote iliyosalia na kumaliza ligi kwa rekodi nzuri kuliko timu zote". Yanga inacheza na Coastal Union jumatano ya wiki hii, mchezo utakaovuta mashabiki wa Yanga kwa wingi ili kushangilia ubingwa, katika mchezo wa awali uliofanyika mwishoni mwa mwaka jana jijini Tanga, Young Africans iliibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Coastal Union mabao yaliyofungwa na washambuliaji Hamis Kiiza na Didier Kavumbagu. Mechi hiyo namba 172 itachezeshwa na mwamuzi Simon Mberwa kutoka Pwani akisaidiwa na Said Mnonga na Charles Chambea wote wa Mtwara wakati mwamuzi wa mezani atakiwa Hashim Abdallah wa Dar es Salaam. Kamishna wa mechi hiyo ni David Lugenge kutoka Iringa. 


Viingilio Yanga vs Coastal union 

Viingilio katika mechi hiyo itakayoanza saa 10.15 jioni ni sh. 5,000 kwa viti vya rangi ya bluu na kijani, sh. 8,000 kwa viti vya rangi ya chungwa, sh. 15,000 kwa VIP C na B wakati VIP A itakuwa sh. 20,000 na tiketi zitauzwa uwanjani siku ya mchezo. Uongozi wa klabu ya Yanga umewaomba wanachama, wapenzi na mashabiki wa timu ya Yanga kujitokeza kwa wingi siku ya jumatano (mei mosi) katika dimba la uwanja wa Taifa ili kuishangilia timu yao na kuendeleza shangwe ya kutwaa Ubingwa wa VPL msimu huu.

Azam FC wameanza mazoezi leo Morocco

Azam FC imetua salama Casablanca Morocco na kusafiri kwa basi umbali wa kilometa 100 hadi Rabat wamefikia katika hoteli ya Golden Tulip mjini Rabat. Wakiwa mjini Rabat Azam leo asubuhi wameanza mazoezi kujiandaa na mechi yao dhidi ya AS FAR timu ambayo inashikilia nafasi ya pili katika msimamo wa ligi kuu nchini Morocco nyuma kwa pointi sita dhidi ya vinara Raja Casablanca wenye pointi 56. AS FAR wamebakiza mechi sita msimu huu wa ligi lakini hadi sasa imefungwa michezo miwili tu na inategemewa kuchukua ubingwa wa Morocco kwani ipo nyuma kwa michezo miwili dhidi ya vinara wa ligi. Katika mchezo wa kwanza uliofanyika jijini Dar es salaam, Azam FC na AS FAR zilitoka droo ya bila kufungana hivyo basi Azam FC inatakiwa kutoka droo yoyote ya magoli au kushinda katika mchezo wake wa marudiano utakaofanyika siku ya jumamosi wiki hii. 

Tutacheza kiwango cha juu kuliko siku zote -Jose



Kocha wa Real Madrid Jose Mourinho amesema leo watacheza katika kiwango chao cha juu kuliko siku zote dhidi ya Dortmund ili kufuzu kwenda fainali. ‘Lazima tucheze katika kiwango chetu cha mwisho, watu wanasema hatuwezi lakini sisi tunataka kuonesha uwezo wetu, jambo hili linawezekana lakini lazima tuwe katika kiwango chetu cha juu ndiyo tutaweza kushinda, hatuwezi kucheza kama tulivyocheza Dortmund, siku ile kiwango chetu hakikuwa kizuri na mabeki wangu hawakuweza kumchezea rafu za kutosha Lewandowski, walimwachia ndiyo maana alituumiza, haiwezekani mchezaji acheze dakika tisini akufunge magoli manne na haujamfanyia rafu hata moja, mabeki wangu walikuwa wazembe, ila safari hii tumejipanga vyema’ hayo yalikuwa maneno ya Jose alipokuwa akihojiwa kusiana na mechi ya leo. Wakati huo huo Ronaldo aliyekuwa majeruhi akisumbuliwa na paja ameruhusiwa na madaktari kucheza mechi ya leo akiwa ndiye mfungaji tegemezi wa Madrid kwani ameshacheza mechi 11 na kufunga magoli 12 kwenye champions ligi. Katika mechi ya leo “mission impossible” Real Madrid wanatakiwa kushinda magoli matatu kwa bila au zaidi dhidi ya Dortmund ili iweze kufuzu kwenda fainali baada ya kufungwa goli 4-1 kwenye mchezo wa kwanza.  

Monday, April 29, 2013

Yanga wanataka makofi ya heshima kwa Coastal

Msemaji wa Yanga bwana Baraka Kizuguto amesema klabu ya Yanga inahitaji kupigiwa makofi ya heshima kama mabingwa wa ligi kuu Tanzania bara mwaka huu. Klabu ya Yanga ambayo imeshatangazwa mabingwa ikiwa wamebakiza mechi mbili, wamehitaji siku ya mechi yao inayofuata dhidi ya Coastal Union wachezaji wa Coastal wapange mistari miwili huku wachezaji wa Yanga wakipita katikati kwa kupigiwa makofi kama wananyofanya kwenye ligi za Ulaya. Kitendo hiki cha kupigiwa makofi ya heshima ni kawaida kufanyika katika ligi za ulaya mfano Man utd walipigiwa makofi na timu ya Arsenal katika mechi ya jumapili iliyopita kama mabingwa wa ligi ya Uingereza mwaka huu. Lakini alipoulizwa katibu mkuu wa TFF bwana Angetile Osiah kuhusiana na jambo hilo alisema Yanga haitaweza kufanyia kitendo hicho kwasababu katiba ya sasa ya TFF hairuhusu kufanya kitendo hicho kwahivyo itakuwa ni vigumu kwa Yanga kupewa heshima hiyo na Coastal Union, ila bwana Osiah amesema jambo hilo ni zuri litazingatiwa ili liwepo kwenye katiba ya TFF. Kitendo hiki cha kupiga makofi ya heshima kimeanzia barani Ulaya ikiwa ni moja ya jitihada ya vyama vya soka duniani kuhamasisha “fair play” hivyo TFF ni vyema wakalifanyia kazi jambo hili kwani mashabiki wa soka Tanzania wanangojea kwa hamu kuona Simba au Yanga inampigia makofi mwenzake, licha yakuwa tukio hilo litakuwa la kihistoria kwenye soka la bongo. 

Tukio hili la kupigiwa makofi ya heshima lilitokea jumapili iliyopita Arsenal walipowapigia makofi Man utd kama mabingwa wa kombe la ligi kuu nchini Uingereza, kitendo kama hiki ndicho Yanga wamehitaji kufanyiwa katika mechi yao inayokuja dhidi ya Coastal Union. 

Mwamuzi afungiwa kuchezesha maisha Russia

Mshika kibendera Musa Kadyrov wa nchini Urusi amefungiwa maisha kuchezesha mechi nchini humo baada ya kumshambulia kwa ngumi na mateke mchezaji wa Amkar Perm, Ilya Krichmar. Musa alifanya kitendo hicho mara tu mwamuzi wa kati kupuliza filimbi ya mwisho kumaliza mchezo. Kijana huyo aliyeshambuliwa alisema ‘ mshika kibendera huyu amekuwa akichezesha vibaya mechi nyingi zikiwemo za kwetu, ila mimi sijawahi kumsema vibaya popote, sasa sijui kwanini alinipiga mimi, nawashukuru wachezaji wenzangu waliokuja kunisaidia, angeniumiza kwa hasira aliyokuwa nayo’. Matukio kama haya ya waamuzi kuwapiga wachezaji ni nadra sana kutokea kwani wao wanasimama kama wasuluhishi wa mchezo hivyo ni kosa kubwa kushiriki katika kuvunja sheria za soka.  
Video ya tukio hilo 

Balotelli atoa kauli nzito kuhusu mpenzi wake

Neguesha, mpenzi wa Balotelli
Mshambuliaji wa Ac Milan Mario Balotelli ametoa kauli nzito baada ya kusema kwamba kama Real Madrid itashinda dhidi ya Dortmund na kuingia fainali atawapatia wachezaji wa Real Madrid mpenzi wake. ‘Kama Real Madrid watashinda magoli mengi na kuingia fainali Wembley basi nitawaachia wachezaji wote wa Real Madrid watoke na mpenzi wangu Fanny Neguesha, nasema hivi kwasababu najua Madrid hawatoki kwa Dortmund’ Mario ameyasema hayo alipokuwa anaongea na gazeti la As Marca. Kauli hii ya Mario imetafsiriwa tofauti na wapenzi wa soka wakisema amemdhalilisha mpenzi wake, kwani sio vyema kufananisha utu au dhamani ya mwanadamu na vitu vya kupita. Ila mashabiki wa Real Madrid nchini Hispania wameipokea kauli hiyo kama chachu ya ushindi, na wamesema watakwenda Italia kumchukua usiku huo huo baada ya ushindi. Real Madrid itashuka dimbani kesho April 30 kupambana na Dortmund katika mchezo wa marudiano jijini Madrid, katika mchezo wa kwanza uliofanyika Ujerumani, Dortmund iliichapa Real Madrid goli 4-1, hivyo Madrid ipo kwenye wakati mgumu kwani itahitajika kushinda magoli matatu kwa bila au zaidi ili kufuzu kuingia fainali. 

Rage aviponda vilabu vya Tanzania

Mwenyekiti wa klabu ya Simba Isamil Aden Rage amesema ni kweli viongozi wa vilabu vya Tanzania hawana malengo ya kushinda vikombe vya kimataifa ikiwemo michuano ya Afrika na Dunia. Rage ameyasema hayo kufatia kauli aliyoitoa mshambuliaji wa TP Mazembe Mbwana Samatta kuwa 'vilabu vikubwa vya Tanzania havina mipango ya kushinda vikombe vya Afrika, wao mipango yao ni kushinda kombe la ligi na kumfunga mpinzani wake'. Katika kuthibitisha hilo Rage amesema kauli ya Mbwana ni ya kweli ndiyo maana vilabu vya Tanzania hutolewa mapema kwenye michuano ya Afrika kwasababu havijajipanga kushindana kimataifa. Rage akiongelea vilabu vya Simba na Yanga ambavyo ndiyo vikubwa, alisema 'mipango ya Simba ni kumfunga Yanga na kuchukua ubingwa, hivyo hivyo kwa upande wa Yanga, kitu ambacho kitaendelea kutufanya tuishie hapa hapa miaka nenda rudi'. Mwaka huu Tanzania imewakilishwa na Simba, na Azam FC kwa upande wa Tanzania bara pamoja na Mafunzo na Super Falcon kwa upande wa Zanzibar, lakini hadi sasa Tanzania imebakiza timu moja tu ya Azam FC ambayo wiki hii itacheza na AS FAR ya Morocco katika mchezo ambao utakuwa mgumu kwa Azam baada ya kutoka droo ya bila kufungana jijini Dar es salaam. 

Nadal na Maria washinda Barcelona na Stuttgart

Rafael Nadal (Kushoto) akiwa ameshikilia kombe aliloshinda katika michuano ya Barcelona open baada ya kumshinda mpinzani wake Nicolas (kulia) kwa seti mbili mfululizo 6-4, 6-3. Hii inakuwa ni mara ya nane kwa Rafael Nadal kushinda Barcelona open ikiwa ni michuano ya nyumbani akiwa kama raia wa Hispania. Nadal aliyekuwa majeruhi kwa muda mrefu ameanza kurudi kwenye kiwango chake licha ya kufungwa na Djokovic katika michuano iliyopita ya Monte Carlo. Nadal ameahidi kufanya vizuri zaidi kwenye michuano inayofuata ya French open ambayo yeye hujigamba kuwa ndiyo michuano yake akiwa anashikilia rekodi ya kushinda mara saba zaidi ya wenzake. 
Maria Sharapova akiwa amekaa juu ya gari aina ya Porsche huku ameshikilia kikombe baada ya kushinda katika michuano ya Stuttgart. Maria ameweza kutetea kikombe hiki baada ya kumfunga Li Na kwa seti mbili mfululizo 6-4,6-3 na kunyakua gari pamoja na kikombe. Maria amesema ushindi huu ni chachu ya ushindi kwenye michuano migumu inayofuata ya French open ambayo wachezaji wote nguli wa tenesi watashiriki. Maria Sharapova kwasasa anashikilia nafasi ya pili duniani kwenye tenesi akiwa na pointi 10240 wakati Serena Williams anashikilia nafasi ya kwanza kwa pointi 11115. 

Rekodi ya tuzo za PFA kuanzia mwaka 1973/74

1973–74
Norman Hunter    - Leeds United
1993–94
Eric Cantona     -  Manchester Utd
1974–75
Colin Todd   -  Derby County        
1994–95
Alan Shearer   - Blackburn Rovers
1975–76
Pat Jennings    - Tottenham H
1995–96
Les Ferdinand    -   Newcastle
1976–77
Andy Gray  -   Aston Villa
1996–97
Alan Shearer     -  Newcastle
1977–78
Peter Shilton   -  Nottingham F     
1997–98
Dennis Bergkamp -Arsenal
1978–79
Liam Brady -    Arsenal
1998–99
David Ginola     -  Tottenham H
1979–80
Liverpool  -   FWA
1999–20
Roy Keane      - Manchester Utd
1980–81
John Wark   -  Ipswich Town        
2000–01
T Sheringham    - Manchester Utd
1981–82
Kevin Keegan   -  Southampton    
2001–02
Ruud van Nistelrooy- Manchester
1982–83
Kenny Dalglish    - Liverpool
2002–03
Thierry Henry     -  Arsenal
1983–84
Ian Rush    - Liverpool    
2003–04
Thierry Henry     -  Arsenal
1984–85
Peter Reid   -  Everton        
2004–05
John Terry      - Chelsea
1985–86
Gary Lineker   -  Everton    
2005–06
Steven Gerrard     -  Liverpool
1986–87
Clive Allen   -  Tottenham H
2006–07
C Ronaldo - Manchester Utd
1987–88
John Barnes   -  Liverpool    
2007–08
C Ronaldo  -Manchester Utd
1988–89
Mark Hughes -    Manchester Utd
2008–09
Ryan Giggs     -  Manchester Utd
1989–90
David Platt   -  Aston Villa        
2009–10
Wayne Rooney  -  Manchester Utd
1990–91
Mark Hughes   -  Manchester Utd
2010–11
Gareth Bale    -   Tottenham H
1991–92
Gary Pallister   -  Manchester Utd
2011–12
Robin van Persie     Arsenal
1992–93
Paul McGrath   -  Aston Villa        
2012–13
Gareth Bale -    Tottenham Hotspur

Kikosi bora cha mwaka ligi kuu ya Uingereza

Gareth Bale ameshinda tuzo ya PFA

Double delight: Gareth Bale won both the Player of the Year and Young Player of the Year awards on Sunday
Gareth Bale akiwa ameshikilia tuzo mbili za mchezaji bora wa mwaka PFA na nyingine ya mcheza bora kijana. Bale anaungana na wachezaji wachache ambao wameshawahi kuchukua tuzo hizi mara mbili akiwemo Cristiano Ronaldo, Mark Hughes, Alan Shearer na Thierry Henry. Mara ya kwanza Bale alishinda tuzo hii mwaka 2010-11
Winners: Bale with Women's Player of the Year Kim Little and PFA Chairman Gordon Taylor
 Picha ya pamoja mchezaji bora wa kike Kim Little, mchezaji bora wa kiume Bale na mwenyekiti wa PFA Gordon Taylor (kushoto)

Sunday, April 28, 2013

Azam FC wamepanda pipa leo kuelekea Morocco

Klabu ya Azam FC leo imesafiri kwenda nchini Morocco kucheza na AS FAR katika mchezo wa marudiano kwenye michuano ya washindi barani Afrika. Katika mchezo wa kwanza uliofanyika jijini Dar es salaam, Azam FC na AS FAR zilitoka droo ya bila kufungana hivyo basi Azam FC inatakiwa kutoka droo yoyote ya magoli au kushinda katika mchezo wake wa marudiano jijini Rabat. Azam FC wameondoka leo na ndege ya shirika la Emirate wakipitia Dubai ikiwa wachezaji wawili wamebaki akiwemo Nuhu Eliye ambaye ni majeruhi pamoja na Ibrahim Shikanda anayeelekea jijini Nairobi nchini Kenya kwenye masomo. 

Jay Z ndani ya Emirates kuwatazama Arsenal

Rapa wa Kimarekani maarufu kwa jina la Jay Z leo alikuwepo katika dimba la Emirates kutazama mechi kati ya Arsenal na Man utd, Jay Z alionekana akiwa na Chris Martin wakitazama mechi iliyokwisha kwa timu hizo kutoka droo ya goli moja kwa moja. Jay Z ambaye alianza kuishabikia Arsenal baada ya kushawishiwa na Thierry Henry tokea mwaka 2010 baada ya Henry kuhamia kwenye klabu ya New York Red Bulls nchini Marekani. Jay Z akiwa ni mwekezaji wa michezo mbalimbali nchini Marekani amekuwa na nia ya kuwekeza kwenye ligi kuu nchini Uingereza husani klabu ya Arsenal hadi sasa Jay Z anafanya tathimini kabla ya kuwekeza kwa klabu hiyo.

Arsenal yapunguzwa kasi na Man utd

Timu za Arsenal na Man utd leo zimetoka droo ya goli 1-1 katika mchezo wa ligi kuu nchini England, Manchester United walishuka dimbani kukamilisha ratiba kwani walishatangazwa mabingwa wa ligi hiyo wiki iliyopita baada ya kushinda goli 3-0 dhidi ya Aston Villa. Lakini kwa upande wa Arsenal mambo bado magumu wakiwa katika kinyang’anyiro cha kuwania nafasi nne za juu ili kupata nafasi ya ushiriki wa klabu bingwa ulaya (UEFA champions). Kwa matokeo ya leo Arsenal wamefikisha pointi 64 wakiwa nafasi ya nne wakati wapinzani wao Chelsea wameshinda mchezo wa leo na wamepanda hadi nafasi ya tatu wakati Tottenham watacheza mechi yao ya 35 tarehe 4 May dhidi ya Southampton. Angalia msimamo wa ligi ulivyo sasa ikiwa utamu wa ligi upo kwa timu hizi tatu za Chelsea, Arsenal na Tottenham.
#Team NamePWDLFAGDPTS
1Manchester United3527447936+4385
2Manchester City3421856131+3071
3Chelsea3419876835+3365
4Arsenal35181076636+3064
5Tottenham3418886043+1762
6Everton35151465238+1459
7Liverpool35141296742+2554
8West Bromwich Albion34146144644+248
9Swansea341012124344–142
10West Ham35119154149–842
11Fulham351010154453–940
12Stoke35913133141–1040
13Southampton35912144757–1039
14Norwich35814133354–2138
15Sunderland34910153845–737
16Newcastle United35107184366–2337
17Aston Villa34810163663–2734
18Wigan3488183962–2332
19Queens Park Rangers35413182956–2725
20Reading35510203765–2825


Here he comes: Van Persie was met with a frosty reception as he walked back onto the pitch at the Emirates
RVP akiingia dimbani pembeni wakiwepo wahudumu wa ndege ya Fly Emirates wadhamini wakuu wa Arsenal ikiwa ni pongezi kwa wachezaji wa Man utd kutwaa ubingwa wa ligi kuu nchini England mwaka 2012/13
Clinical: Theo Walcott put Arsenal a goal to the good after just two minutes
Walcott akifunga goli pekee la Arsenal

Blast from the past: Arsenal fans watched Robin van Persie net from the spot for United to equalise
RVP akifunga goli la kusawazisha kwa penati