Thursday, April 25, 2013

Ferguson atenga paundi mil 30 kwa Lewandowski

Baada ya Lewandowski kupachika goli nne kwenye mechi ya nusu fainali kati ya Dortmund na Real Madrid, kocha wa Man utd Sir Alex amezidi kuvutiwa na mchezaji huyo kiasi cha kutenga bajeti ya paundi milioni 30 ili kumnasa mshambuliaji huyo wa Borussia Dortmund. Hadi jumatano ya wiki hii Man utd ilikuwa bado haijaridhishwa kwa asimilia mia moja na kiwango cha Lewandowski kiasi cha kumtuma mshauri mmoja wa Sir Alex kwenda Ujerumani kumwangalia mchezaji huyo akicheza mechi dhidi ya Real Madrid, lakini baada ya mechi hiyo ripoti ya mshauri wa Sir Alex ilionesha kuridhishwa na kiwango cha mchezaji huyo kiasi cha kumwekea bajeti ya paundi mil 30 ili kumsajili Lewandowski akiwa ndiyo chaguo namba moja la Ferguson katika msimu ujao wa usajili. Mbali ya United, PSG na Bayern Munich pia zimekuwa zikimuwinda mshambuliaji huyo kwa karibu zaidi ili kuimarisha vikosi vyao ila Man utd na Bayern ndiyo timu zilizopo kwenye nafasi nzuri kumnasa Lewandowski zaidi ya PSG timu ambayo bado hajavutiwa nayo. Lewandowski hadi sasa ameshacheza mechi 9 kwenye michuano ya UEFA na kufunga magoli 10 wakati kwenye ligi ya Ujerumani anaongoza kwa ufungaji wa magoli 23 hadi sasa.  

No comments:

Post a Comment