Tuesday, March 26, 2013

Big mechi leo France vs Spain


Leo usiku kutakuwa na mechi nzuri ya kuangalia kati ya France na Spain. Timu zote ni nzuri na zina wachezaji wanaocheza kwenye ligi kubwa barani ulaya. Katika kundi “I” France anaongoza kwa kuwa na pointi 10 akifuatiwa na Spain pointi 8. Kwenye mchezo wa leo Spain wamekamia kushinda ili kurudisha matumaini ya timu yao baada ya kulazimishwa droo na Finland ijumaa iliyopita kwenye uwanja wa nyumbani. Utamu wa mechi ya leo ni kuona nani anakwenda kilele kwenye kundi “I” vile vile Spain na France wote wanajua kucheza mpira wa kuvutia, tutaona nani mbabe.Vikosi vya Spain na France vinatarajiwa kuwa kama ifuatavyo 
France: Lloris, Jallet, Varane, Sakho, Evra, Pogba, Matuidi, Cabaye,Valbuena, Benzema, Ribery
Spain: Valdes, Arbeloa, Pique, Ramos, Monreal, Xavi, Busquets, Alonso, Pedro, Fabregas, Iniesta

No comments:

Post a Comment