Tuesday, March 26, 2013

WWC chachu ya ushindi Arsenal

Wilshere, Walcott na Cazorla (WWC) wametajwa kuwa wachezaji muhimu sana kwa Arsenal. Wachezaji hawa wanacheza nafasi ya kiungo na ushambuliaji wamekuwa ni chachu kubwa ya ushindi kwenye timu ya Arsenal. Arteta ni mchezaji mzuri na ana uwezo mzuri wa kumili na kugawa mipira lakini kurudi kwa Wilshere na usajili wa Cazorla umefanya Arteta asionekane akiwa kiwanjani. Kocha wa Arsenal Arsene Wenger amekuwa kwenye mazungumzo mara kadhaa na kocha wa England Hodgson ili kumshawishi asiwatumie sana Walcott na Wilshere kwenye michezo ya kirafiki ili kuwapa muda wa kupumzika na kupunguza riski ya kuumia kwani kukosekana kwao uwanjani ni pigo kubwa kwa Arsenal. Katikati ya msimu huu kulizuka tetesi kuwa Walcott anaweza kuhama Arsenal, lakini uongozi wa Arsenal kwa kutambua umuhimu wake waliweza kumbakiza kundini. Ki-ukweli hawa wachezaji ni wakali, Arsene Wenger akikubali kubadilisha sera zake za kuuza wachezaji wakubwa basi Arsenal itakuwa inatisha sana misimu ijayo. 

No comments:

Post a Comment