Monday, March 25, 2013

Nataka kushinda UEFA na timu ya England - Mourinho


Jose Mourinho anatarajiwa kurudi Stamford Bridge hivi karibuni kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo urafiki mzuri aliokuwa nao na Bosi wa Chelsea Abramovich. Vile Vile wiki iliyopita Mourinho alisikika akisema anahamu ya kushinda UEFA na timu ya England, akiulizwa timu gani atayoweza kuhamia alisema ni siri yake, ila alikiri kuwa akitoka Madrid atahamia England, Mourinho alisema“ Siwezi kuficha kitu, ni kweli baada ya Spain nakwenda England, hilo lipo wazi, nimekuwa nikiliongelea hili mara nyingi na nitaendelea kuliongelea, siwezi kuficha kitu. Mourinho amekuwa akihusishwa sana na Man utd, lakini uwepo wa Sir Alex inasemekana unamzuia Mourinho. DailyMail, limeripoti kuwa hivi karibuni bosi wa Chelsea Abramo amekuwa karibu zaidi na Mourinho ikizingatiwa kuwa Rafa Benitez muda wake wa kuifundisha Chelsea unakaribia kuisha. Abramo anapenda kocha mwenye uhakika wa kuijenga timu na kuipa timu ushindi ikiwa Mourinho ndiyo chaguo lake la kwanza.  

No comments:

Post a Comment