Tuesday, March 26, 2013

Obama awapongeza Galaxy kwa ushindi


Obama amewapongeza Galaxy kwa kushinda  kombe la MLS kwa mara ya pili mfululizo, Obama alitoa pongezi hizo wakati akiwatakia heri wachezaji wa timu ya taifa katika mechi yao na Mexico. Obama alisema nawapongeza sana Galaxy kwa ushindi, mtawapa salamu zangu wachezaji wenzenu ambao hawapo hapa, najua wao pia wapo kwenye timu zao za taifa wakitekeleza majukumu ya kitaifa. Obama pia alipewa jezi pamoja na mpira wa Galaxy kama shukrani na zawadi kutoka kwa Landon Donovan akiwakilisha club yake. 

No comments:

Post a Comment