Tuesday, April 16, 2013

Bifu la Terry na Benitez bado linaendelea

Torres, Terry na Lampard wakiwa benchi dhidi ya Man city
Beki mkongwe wa Chelsea John Terry ameikana kauli ya kocha wake Rafa Benitez kuwa yeye hawezi kucheza mechi mbili kwa wiki. Terry ameyasema hayo baada ya Benitez kusema kuwa Terry asingeweza kucheza kwenye mechi dhidi ya Man city kwasababu alikuwa mgonjwa na hali yake haimruhusu kucheza mechi zaidi ya mbili kwa wiki. Akimjibu kocha wake John Terry alisema “mimi nimeshapona naweza kucheza mehi zaidi ya mbili kwa wiki, maneno aliyosema kocha sio ya kweli”. Benitez na Terry wamekuwa kwenye mgogoro kwa muda mrefu sasa tokea mwezi wa pili baada ya Chelsea kufungwa na Man city katika mchezo wa ligi kuu, mgogoro wao ulisababishwa na mfumo mpya aliouleta Benitez ambao Terry alitofautiana nao. Tesisi zinasema Benitez anatumia kigezo cha Terry kuwa mgonjwa ili asicheze ila kiukweli bifu lao ndiyo chanzo cha Terry kukaa benchi, vilevile, Frank Lampard pia anahusishwa na bifu la chini chini dhidi ya Benitez mambo ambayo yanamponza Benitez nakumfanya ampoteze mechi ambazo angeweza kushinda.  

No comments:

Post a Comment