Tuesday, April 16, 2013

Ligi kuu Tanzania bara Yanga,Mtibwa,Kagera uwanjani

Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kuwania ubingwa wa Tanzania Bara inaendelea kesho Aprili 17 mwaka huu kwenye viwanja vitatu huku vinara wa ligi hiyo Yanga inayoongoza kwa pointi 52 itakuwa mgeni wa Mgambo Shooting katika mechi itakayochezeshwa na mwamuzi Athuman Lazi kutoka Morogoro kwenye Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga. Kagera Sugar na Toto Africans zitaumana kwenye Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba wakati uwanja wa Manungu ulioko Turiani mkoani Morogoro itazikutanisha mwenyeji Mtibwa Sugar yenye pointi 33 na Oljoro JKT yenye pointi 28. Mechi mbili za kesho ndizo zinaonekana kuwa ni ngumu kutokana na msimamo wa ligi ulivyo hivi sasa kwani Yanga inahitaji pointi tano tu ili iweze kutwaa ubingwa wakati huo huo Mgambo itakuwa inahitaji ushindi ili iweze kuepuka kushuka daraja. Mechi nyingine ngumu ni kati ya Kagera na Toto, Kagera wenyewe poinit 37 wahitaji ushindi ili waweze kuishika nafasi ya tatu wakishindana na Simba, wakati Toto watahitaji kushinda ili kuepuka kushuka daraja. Ufuatao ni msimamo wa ligi kwasasa.
RankTeamsPlayedWinsDrawLostGDPoints
1Young Africans2216422852
2Azam FC2314542247
3Kagera Sugar221075737
4Simba SC229941136
5Mtibwa Sugar23896233
6Coastal Union22886332
7Ruvu Shooting22868030
8JKT Oljoro23779-428
9Prisons FC246810-726
10Mgambo Shooting227312-724
11Toto African2441010-1122
12JKT Ruvu216411-1522
13Police M2331010-1019
14African Lyon235414-1919

No comments:

Post a Comment