Saturday, April 13, 2013

Sina uhakika na namba - Lampard

Kiungo wa Chelsea Frank Lampard amesema wachezaji wengi wa Chelsea akiwemo yeye hawana uhakika wa namba. Lampard akinukuliwa na The Daily Telegraph amesema “sidhani kama kuna mchezaji wa Chelsea ukiondoa golikipa na mabeki wenye uhakika wa kucheza mechi yoyote. Mimi nimekuwa kwenye kiwango cha juu sana hivi sasa lakini sina uhakika kama nitacheza dhidi ya Man City, jambo hili linategemea na mapenzi ya kocha na mahusiano kati ya mchezaji na kocha”. Lampard alimalizia kwa kusema “Napenda sana kucheza mechi zote za Chelsea lakini kocha ndiye mwenye maamuzi ya mwisho kuchagua nani wa kucheza”. Wachambuzi wa maswala la soka wamesema kauli hii ya Lampard imeonesha wazi kuwa kiungo huyu hana mahusiano mazuri na kocha wake Benitez jambo ambalo linakoleza zile tetesi  kuwa Lampard atahamia Galaxy ya Marekani msimu ujao. Chelsea inashuka dimbani jumapili kukutana na Man City katika mchezo wa nusu fainali ya FA, mchezo utakao fanyika kwenye uwanja wa Wembley.  

No comments:

Post a Comment