Sunday, July 7, 2013

'Sina wasiwasi na ujio wa Higuain' - Podolski

Mshambuliaji wa Arsenal, Lukas Podolski amesema haogopi kukosa namba kweye kikosi cha kwanza hata kama Gonzalo Higuain atajiunga na klabu hiyo. Podolski ameyasema hayo alipokuwa akiongea na The Sun akisema ‘wakati wote ni vyema kuona wachezaji wazuri wanasajiliwa, mimi sina wasiwasi wowote kwasababu najiamini ni mchezaji mwenye nguvu na uwezo mzuri. Wachezaji wazuri wakija nafurahi, kwasababu nitacheza vizuri zaidi. Mambo haya yakifanikiwa, msimu ujao Arsenal tutakuwa kamili na tutacheza kushindania ubingwa pamoja na klabu kubwa zingine. Natambua ugumu wa ligi ikizingatiwa kwamba klabu zingine zina makocha wapya, lakini, Arsenal tutakuwa washindani wao wakubwa msimu ujao, na uzuri wa ligi ya England kabla ya ligi kuisha mshindi hajulikani tofauti na Hispania ambapo mshindi ni Barcelona na Madrid wakati wote’. Podolski ameyasema hayo huku hatua za usajili wa Higuain na klabu ya Arsenal zikiwa kwenye hatua za mwisho mwisho na taarifa zinasema Arsenal na Madrid wanatarajia kumalizana wakati wowote na Higuain atatua Emirates. 

No comments:

Post a Comment