Tuesday, March 26, 2013

Humud kuelekea Jomo Cosmos wikiendi hii


Kiungo mwenye mapafu ya mbwa Abdulhalim Humud Gaucho huenda akasafiri kuelekea bondeni Afrika ya Kusini wikiendi hii kufuatia kupata nafasi ya majaribio kwenye timu ya Jomo Cosmos aliyowahi kuchezea Nteze John na Ally Shah siku za nyuma. Cosmos inayomilikiwa na kocha wa zamani wa Bafana Bafana Jomo Sono imempa nafasi hiyo Humud baada yakufanyiwa mipango na uongozi wa Azam FC katika kutekeleza sera yake ya kutengeneza uwanja mkubwa kwa wachezaji wa kitanzania kwenye ligi mbalimbali zinazoendeshwa kisasa. Taarifa hizi ni kwa mujibu wa Azam FC.

No comments:

Post a Comment