Tuesday, March 26, 2013

Guardiola aliniomba ushauri- Luca Toni


Luca Toni mshambuliaji wa Fiorentina amekiri kuwa kocha wa zamani wa Barcelona Pep Guardiola alimuomba ushauri kuhusu kuhamia Bayern Munich. Pep na Toni walikuwa timu moja mwaka 2001 na 2003 walipokuwa wakichezea club ya Brescia. Guardiola alimuomba ushauri Toni kwasababu alishachezea club ya Munich mwaka 2007 hadi 2010 na kuweza kushinda kombe moja la Bundes. Toni alisema “Pep aliniita mahali na akaniuliza vipi Munich kukoje, vipi hali ya maisha ndani ya club, nilimjibu vyema na uamuzi wake kwenda Bayern ulinipa furaha. Pep Guardiola mwishoni mwa mwaka jana alifunga mkataba na Munich ambao utaanza mwanzoni mwa msimu ujao. Fununu zinasema Pep ameshaomba fungu kubwa la usajili na kuwataja wachezaji anaowahitaji akiwemo Suarez, Mata na Naymer. 

No comments:

Post a Comment