Friday, March 22, 2013

Walcott majeruhi, hatoweza kucheza leo dhidi ya Marino

Theo Walcott winga wa Arsenal ameumia jana usiku kwenye mazoezi hivyo hatoweza kucheza mechi kati ya England na San Marino. Walcott anatarajiwa kurudi nchi England katika club yake ya Arsenal ili aweze kufanyia matibabu. Theo alitarajiwa kucheza mechi ya leo na ijayo lakini haitowezekana kwani imekisiwa kuwa atachukua wiki mbili hadi tatu kupona. England inacheza leo na San Marino kwenye mchezo wa kufuzu kombe la dunia 2014 nchini Brazil. 

No comments:

Post a Comment