Wednesday, April 17, 2013

Aguero kaomba msamaha kwa Luiz

Mshambuliaji wa Man City Sergio Aguero amemwomba radhi David Luiz wa Chelsea baada ya kumfanyia rafu mbaya katika mchezo wa nusu fainali kati ya Chelsea na Man city wikiendi iliyopita. Aguero alitakiwa kupewa kadi nyekundu katika mchezo huo lakini mwamuzi hakuweza kutoa adhabu hiyo jambo ambalo lilisababisha mzozo kwa mashabiki wa Chelsea lakini Aguero alitambua makosa yake na amekiri kuwa alimfanyia rafu mbaya Luiz. Aguero alimuomba msamaha Luiz kwa kumpigia simu na kukubaliana, baada ya kukubaliana kwenye simu Aguero na Luiz walimalizia maongezi yao kwenye twitter ambapo Aguero alisema “Nimewasiliana na Luiz na nimemuomba msamaha kwasababu nilifanya rafu ambayo sikukusudia” naye Luiz alijibu kwa kusema “nakushukuru Aguero kwa ujasiri na utu ulioonesha”. Mbali na msamaha alioupata Aguero kutoka kwa Luiz, FA pia imesema haitatoa maamuzi yoyote kufuatia rafu hiyo kwani sio rafu ambayo ilikuwa inahitaji maamuzi ya nje ya uwanja. 

No comments:

Post a Comment