Wednesday, April 17, 2013

Waziri wa michezo aunda kamati ya ushindi Taifa Stars

Waziri wa Habari Utamaduni na Michezo Dk. Fenella Mukangara ameunda kamati ya wajumbe kumi na moja (11) itakayokuwa na kazi ya kuhakikisha timu ya Taifa (Taifa Stars) inashinda. Taifa Stars iliyopo kwenye nafasi nzuri ya kufuzu kucheza kombe la dunia nchini Brazil mwaka 2014 inahitaji kuendeleza ushindi ili iweze kufuzu. Katika kuhakikisha inapata ushindi waziri wa michezo ameamua kuunda kikosi kazi kinachojumusha wajumbe kumi na moja ambao Mohamed Dewji (Mb), Mkuu wa ZSSF Dk Ramadhani Dau, Rais wa TFF Leodegar Tenga, Mwenyekiti wa BMT Dioniz Malinzi, Zitto Kabwe (Mb), George Kavishe, Mohamed Raza (Mb), John Komba (Mb), Teddy Mapunda, Abji Shabir na Joseph Kusaga. Hakika hii ni timu kazi kwani imehusisha wajumbe wengi ambao ni wapenda soka na wenye fursa mbalimbali zinazoweza kuisaidia Stars kushinda katika mechi zake zilibakia. 

No comments:

Post a Comment