Wednesday, April 17, 2013

Yanga yalazimishwa droo ya goli 1 - 1 na Mgambo

Timu ya Yanga leo imetoka droo ya goli moja kwa moja na timu ya Mgambo katika mechi iliyofanyika katika uwanja wa mkwakwani jijini Tanga. Kwa matokeo haya Yanga inaendelea kushika nafasi ya kwanza ikiwa na pointi 53 licha ya kujipunguzia kasi kuelekea kwenye ubingwa wa ligi kuu. Kama Yanga ingeshinda mechi ya leo ingebakiza pointi mbili tu ili kunyakuwa ubingwa, ila kwa matokeo ya leo umeifanya Yanga ibakize pointi nne kuchukua ubingwa katika michezo mitatu iliyobakia.  

No comments:

Post a Comment