Wednesday, April 17, 2013

Cardiff ni timu ya kwanza kuingia ligi kuu BPL

Cardiff imekuwa ni timu ya kwanza kuingia ligi kuu ya Uingereza baada ya kutoka sare ya bila kufungana dhidi ya Charton katika mechi iliyofanyika jana usiku. Cardiff imeweza kufikisha pointi 84 pointi ambazo zinaweza kufikiwa na timu moja tu ya Hull City. Kutoka ligi ya championship timu tatu tu ndiyo zinatakiwa kupanda daraja, hivyo timu moja imeshapatikana na zimebakia timu mbili ambapo hadi sasa mchuano mkali upo kwenye timu tatu za Hull city, Watford na Brighton ambazo zinawania nafasi mbili zilibakia. Ukiangalia msimamo kwenye jedwari hapo chini utaona tofauti ndogo ya pointi kati ya timu hizi ambazo zimebakiza michezo mitatu kila mmoja. Cardiff yenye udhamini wa 1Malaysia imeweza kuingia ligi kuu baada ya miaka 51 jambo ambalo ni la kihistoria kwenye mji wa Cardiff City.

No comments:

Post a Comment