Monday, April 15, 2013

Nimerudi kwenye 'fomu' - Nasri

Kiungo wa Man City Samir Nasri amemwambia kocha wake Roberto Mancini kuwa kwasasa amerudi kwenye kiwango chake. Nasri alisema hayo alipokuwa akiongea na SportsVibe “nimeshamwambia Mancini kuwa nipo 'fiti' na hata yeye amekubaliana na mimi, nilikuwa nasumbuliwa na maumuvi kwa kipindi sasa, lakini nimerudi kwenye “fomu”. Natamani sana ningekuwa nacheza hivi tokea mwanzo wa msimu ili niisaidie timu yangu, lakini sikuweza kwasababu nilikuwa majeruhi, ila nimerudi naamini nitaisaidia City kwa kipindi hiki kilichobakia kwenye michezo ya ligi na FA cup. Katika mchezo wa jana (Man city na Chelsea) nusu fainali ya FA cup Nasri alionesha mchezo mzuri akiwa amefanikisha pasi 38 kati ya 49 na pia alifunga goli la kwanza baada ya kuwapiga chenga mabeki wa Chelsea.    
Nasri akipangua ngome ya Chelsea kabla ya kufunga goli katika mchezo wa nusu fainali kati ya Man City na Chelsea, mchezo uliokwisha kwa Man City kuibuka na ushinda wa goli 2-1

No comments:

Post a Comment