Baada ya kutwaa ubingwa, klabu ya Manchester United usiku wa
jumatano ilifanya sherehe za kuwatunuku wachezaji waliofanya vizuri msimu huu.
Michael Carrick ndiye alitoka kinara kwenye tuzo hizo baada ya kupata tuzo ya
mchezaji bora wa mwaka, wakati Robin Van Persie aliweza kupata tuzo mbili moja
ya goli bora alilofunga dhidi ya Aston Villa na nyingine ya mchezaji
aliyependwa na mashabiki. Adnan Januzaj alipata tuzo ya mchezaji kijana na Ben
Pearson alipata tuzo mchezaji bora wa akademi. Shughuli hii ya kutoa tuzo ilikwenda sambamba na sherehe kubwa ambapo wachezaji wa Man utd, wake/wachumba zao pamoja na viongozi wa klabu walijumuika pamoja kusherehekea mafanikio yote kwa ujumla ya klabu hiyo msimu huu.
|
Carrick akipokea tuzo ya mchezaji bora wa mwaka |
|
RVP naye alipokea tuzo yake ya goli bora dhidi ya Aston Villa |
|
RVP na Sir Alex wakisalimiana kabla ya party kuanza, imesemeka kuwa RVP ndiye mchezaji anayependwa zaidi na Babu kwasasa. |
|
Adnan Januzaj akipokea tuzo ya mchezaji kijana |
|
Wachezaji wakiingia ukumbini, Rooney kama kawaida hakuna kutabasamu, bado ana kabifu na Sir Alex baada ya kugomewa kuhama |
Mitindo ilikuwepo pia, chagua aliyetokelezea zaidi
No comments:
Post a Comment