Klabu ya Chelsea imeweza kuweka rekodi barani ulaya baada ya jana kutwaa ubingwa wa Europa cup ikiwa ni mara mbili mfululizo kushinda vikombe viwili vya ulaya baada ya mwaka jana kushinda kombe la UEFA champions. Chelsea inakuwa ni timu pekee ambayo imeweza kutwaa makombe haya mawili kwa miaka inayofuatana tofauti na timu zingine ambazo zimeshawahi kushinda makombe haya lakini kwa miaka mbalimbali. Chelsea iweza kushinda kombe hili baada ya kuifunga Benfica ya Ureno kwa goli 2-1, magoli yaliyofungwa na Torres na Ivanovic. Ushindi huu unawapa kigugumizi viongozi wa Chelsea kuhusu Benitez, kocha ambaye wanatarajia kumfukuza na nafasi yake kuchukuliwa na Mourinho. Hongera Chelsea
No comments:
Post a Comment