Sunday, May 19, 2013

Liewig aipongeza Yanga kwa ushindi

Kocha wa klabu ya Simba Patrick Liewig amesema kikosi cha Yanga kinastahili pongezi baada ya kushinda mchezo wa jana a goli 2-0. Liewig aliyasema hayo wakati akihojiwa baada ya mchezo na kusema “ Yanga walistahili ushindi kwenye mchezo wa leo kwasababu kikosi chao kilikuwa bora kwa kipindi kizima cha ligi kuu tofauti na kikosi changu cha Simba ambacho nimeanza kukijenga upya miezi miwili tu kabla ya mchezo wa leo” . Hata hivyo Liewig aliwasifia vijana wake kwa kujitahidi kupambana tokeo mwanzo wa mchezo hadi mwisho na kusema Simba wanajipanga kwa msimu ujao ili kurekebisha makosa yaliyojitokeza msimu huu. Kwa matokeo ya jana ambapo Simba ilifungwa goli 2-0 na Yanga imeifanya Yanga imalize ligi na pointi 60 tofauti ya pointi 15 dhidi ya Simba yenye pointi 45. 

No comments:

Post a Comment