Sunday, May 19, 2013

Beckham atoa machozi mechi ya mwisho

David Beckham jana usiku alitoka kiwanjani huku akilia ikiwa ndiyo mechi yake ya mwisho kucheza baada ya kutangaza kustaafu. Beckham alitolewa kwenye kipindi cha pili dakika ya 82 akibadilishana na Lavezzi. Beckham, baada ya kuona kibao kimeonesha yeye ndiye anatoka, alianza kukumbatiana na wachezaji wenzake huku machozi yakimtoka na kutembea hadi kwenye benchi lakini baada ya mchezo kuisha haikuwa tena kilio , wachezaji wa PSG pamoja na Beckham walianza kusherekea ndani ya uwanja wakimuaga mwenzao.

Teary: David Beckham burst into tears when he realised he was to be substituted by Carlo Ancelotti
Mtu mzima alishindwa kujizuia, anakumbukia enzi zake za kila faulo goli, sasa ni muda wa kuwaachia kijiti wengine inamuuma sana 
Upset: David Beckham applauded the fans as he left the pitch in tears after being substituted
Atakumbukwa daima kwa utalaamu wake wa kupiga mipira ya faulo, kona na pasi ndefu.
Moving: The PSG players hugged Beckham as he was substituted
Moving: The PSG players hugged Beckham as he was substituted
Custom made: Beckham wore these adidas boots on his final game at the French club
Beckham alivaa viatu vyenye majina ya watoto wake maalumu kwa ajili ya mechi yake ya mwisho (watoto wake ni Brooklyn, Romeo, Cruz na Harper)
Thanks boss: Carlo Ancelotti and Beckham share a moment as he leaves the pitch
Beckham akimkumbatia kocha huku akitoa machozi baada ya kutolewa dk 82


Baada ya mechi kuisha ilikuwa ni sherehe sio vilio tena 

Proud: David Beckham was joined by his three sons with the Ligue 1 trophy after helping PSG to victory
Beckham akiwa na watoto wake  Brooklyn, Romeo na Cruz
Up you go: After the final whistle, Beckham was flung into the air by his team-mates
Wachezaji wa PSG wakimpongeza Beckham kwa kumrusha juu baada ya mechi, kilio chote kilikata
Moving: Beckham put the English flag around his neck for a lap of honour after the match
Beckham akiwa na bendera ya Uingereza kuonesha utaifa baada ya mechi
Moving: Beckham put the English flag around his neck for a lap of honour after the match
Alipewa tuzo kama shujaa baada ya kucheza kwa muda mrefu
No 1 fan: Victoria Beckham arrives at the stadium in Paris to watch her husband
Victoria mke wa Beckham pia alikuwepo kiwanjani

No comments:

Post a Comment