Klabu ya Malaga leo imethibitisha kuwa kocha Manuel Pellegrini alishaomba kuhama
mwishoni mwa msimu huu na yupo huru kuondoka. Uongozi wa Malaga umesema hayo
baada ya uvumi kuwa kocha huyo yupo kwenye mazungumzo ya mwisho na klabu ya Man
city ili kuchukua nafasi ya Mancini. Katika ripoti yake, klabu ya Malaga imesema
Pellegrini yupo huru kuondoka bila ya kulipa pesa zozote hata kama mkataba wake
unakwisha baada ya miaka miwili ijayo. Vilevile, taarifa za wiki hii zinasema
Man city wameshaongea na Pellegrini na wapo kwenye hatua za mwisho kufikia
makubaliano hivyo siku yoyote watamtangaza rasmi kuwa kocha mpya wa klabu hiyo.
No comments:
Post a Comment