Roger Federer akiwa mwenye huzuni baada ya kutolewa na Tsonga kwa seti 7-5, 6-3, 6-3 kwenye michuano ya French Open. Federer ambaye ni bingwa wa Grand Slams 17, amekuwa akifanya vibaya mara zote kwenye michuano inayofanyika viwanja vyenye vumbi ikiwemo French Open na imekuwa ni udhaifu wake wa muda mrefu jambo ambalo linamfanya mpinzani wake Rafel Nadal kushinda Slams nyingi za michuano ya French open kwasababu hana mpinzani. |
Tsonga akishangilia baada ya mechi kuisha akiwa haamini kumtoa mchezaji bora namba mbili duniani Roger Federer kwa seti tatu mfululizo. Kwa matokeo haya Tsonga atakutana na David Ferrer kwenye nusu fainali itakayofanyika Juni 7.
Serena ashinda dhidi ya mpinzani wake Kuznetsova
Serena akishangilia kwa machungu baada ya kumbwaga mpinzani wake kwenye michuano ya French open Svetlana Kuznetsova kwa seti 6-1, 3-6, 6-3 kwenye mechi iliyokuwa na upinzani huku Serena na Svetlana wakioneshana viwango vya hali ya juu.
Svetlana Kuznetsova akirudisha mpira kwa nyuma 'Backhand'. Kuznetsova mara nyingi huwa anamfunga Serena hadi analia uwanjani lakini safari hii amepatiwa dawa yake
Angalia viwango vya tenesi kwenye highlights za mechi zote mbili
Svetlana Kuznetsova akirudisha mpira kwa nyuma 'Backhand'. Kuznetsova mara nyingi huwa anamfunga Serena hadi analia uwanjani lakini safari hii amepatiwa dawa yake
Angalia viwango vya tenesi kwenye highlights za mechi zote mbili
No comments:
Post a Comment